Posts

Showing posts from June, 2026

INDICATIVE EXCHANGE RATES TODAY JUNE 4th, 2026

Image
 

WFP KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

Image
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula la Duniani (World Food Programme -WFP) limesema litaendeleza mashirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha masuala ya menejimenti ya maafa yanaendelea kutekelezwa kwa tija na malengo yaliyokusudiwa kwa kuimarisha uwezo wa kitaalamu na Kiteknolojia kwa kutumia teknolojia za kisasa. Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi wa WFP Tanzania Bi. Christine Mendes wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura inayoendelea mkoani Morogoro. Bi.Christine alisema ushirikiano hususan katika kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji. Aidha, alieleza kuwa zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wak...

SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA ZA WILAYA KUIMARISHA UCHUMI: MSIGWA

Image
  Mwanza Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara nchini kwa kupunguza barabara za changarawe na kujenga barabara za lami katika wilaya mbalimbali, hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kuinuka kiuchumi kupitia shughuli za usafirishaji. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alipokuwa akizungumza na Maofisa Uhusiano na Mawasiliano Serikalini wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Chama cha Maofisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) unaoendelea jijini Mwanza. Msigwa amesema maofisa Mawasiliano wanapaswa kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali kwa kuwa miradi hiyo ni ya manufaa kwa wananchi wenyewe. “Sisi ndiyo tunaobeba taswira ya Serikali. Tunapaswa kuwaonesha wananchi fursa zilizopo kutokana na uwekezaji mkubwa wa miundombinu unaofanywa na Serikali,” amesema. Ameongeza kuwa Serikali imejenga barabara za mzunguko zenye urefu wa kilomita 56 k...

RAIS SAMIA AKUTANA NA VLADIMIR PUTIN MOSCOW, WAWEKA MKAKATI MZITO WA DIPLOMASIA

Image
MOSCOW, URUSI – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 03 Juni, 2026, amewasili katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow nchini Urusi kwa ajili ya ziara ya kiserikali yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili. ​Mara baada ya kuwasili Ikulu hapo, Rais Samia alilakiwa na mwenyeji wake, Rais wa Shirikisho la Urusi, Mhe. Vladimir Putin, ambapo viongozi hao wawili walisalimiana na kupiga picha ya pamoja kabla ya kuelekea kwenye meza ya mazungumzo. ​Katika ziara hiyo, Rais Samia ameongoza ujumbe mzito wa viongozi na wataalamu kutoka Tanzania katika mazungumzo rasmi na Rais Vladimir Putin pamoja na ujumbe wake wa Serikali ya Urusi. ​Mazungumzo hayo yaliyofanyika ndani ya Ikulu ya Kremlin yamelenga kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu katika nyanja za kimkakati ikiwemo biashara, uwekezaji, teknolojia, na diplomasia ya kimataifa, huku yakifungua milango mipya ya maendeleo kwa pande zote mbili.

MAAFISA 2,028 KUPANDISHWA VYEO: IDARA YA UHAMIAJI YAWEKA REKODI MPYA SERIKALINI

Image
  ‎Katika jitihada za kuendelea kuimarisha utendaji kazi wa taasisi za umma na kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi, Serikali imeendelea kutekeleza sera ya kuwathamini na kuwatambua watumishi kupitia upandishaji vyeo kulingana na sifa, uzoefu na utendaji wao wa kazi. Hatua hiyo imeendelea kuleta matokeo chanya katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na taasisi zake, ikiwemo Idara ya Uhamiaji. ‎Kwa mujibu wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, jumla ya watumishi 9,689 wa Wizara na taasisi zake walipandishwa vyeo.  ‎Kati ya hao, watumishi 693 wa Idara ya Uhamiaji walinufaika na hatua hiyo, jambo linalodhihirisha dhamira ya Serikali ya kuendelea kuwatambua watumishi wanaotekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na kujituma. ‎Katika mwaka wa fedha 2026/27, Serikali imepanga kuendelea kuimarisha ustawi wa watumishi wake kwa kuwapandisha vyeo jumla ya watumishi 23,089 wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nch...

BEI YA PETROLI YASHUKA, SERIKALI YAWEKA RUZUKU KWENYE DIZELI

Image
  Watumiaji wa petroli wamepata afueni mwezi Juni 2026 baada ya bei ya mafuta hayo kushuka ikilinganishwa na mwezi uliopita. Kwa Dar es Salaam, petroli sasa itauzwa kwa bei kikomo ya shilingi 4,086 kwa lita, hatua inayotarajiwa kupunguza gharama kwa watumiaji wa kawaida na baadhi ya shughuli za usafiri. Kwa upande wa dizeli, watumiaji wanakabiliwa na ongezeko dogo la bei, ambapo kwa Dar es Salaam bei kikomo imefikia Shilingi 4,333 kwa lita. Ongezeko hilo limechangiwa na kupanda kwa gharama za mafuta katika soko la dunia pamoja na kuongezeka kwa gharama za uagizaji wa bidhaa hiyo. Licha ya changamoto hizo za kimataifa, Serikali imeendelea kuchukua hatua za kulinda uchumi na wananchi kwa kuweka ruzuku ya Shilingi 534.91 kwa kila lita ya dizeli. Hatua hiyo imelenga kupunguza athari za ongezeko la bei kwa sekta muhimu kama usafirishaji, viwanda na huduma za kijamii. Mabadiliko haya yameathiriwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea Mashariki ya Kati, vinavyohusisha Marekani, Israeli...

UNICEF YAIMWAGIA SIFA TANZANIA SEKTA YA MAJI, YAMWAGA DOLA MILIONI 11.5 KUIMARISHA HUDUMA ZA WASH

Image
  Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) limeipongeza Tanzania kwa kuendelea kupiga hatua kubwa katika kuboresha huduma za maji na usafi wa mazingira, hatua zinazotokana na uwekezaji mkubwa unaofanywa na Serikali katika sekta hiyo na kuifanya nchi kuendelea kung’ara barani Afrika na duniani. Pongezi hizo zimetolewa na Mwakilishi wa UNICEF nchini, Bi. Elke Wisch, wakati wa mazungumzo na viongozi wa Wizara ya Maji yaliyofanyika katika Makao Makuu ya Wizara ya Maji – Mtumba, jijini Dodoma meo tarehe 2 June 2026.  Mazungumzo hayo yalilenga kutathmini mafanikio ya ushirikiano uliopo na kujadili maeneo mapya ya ushirikiano yatakayochangia maendeleo zaidi ya sekta ya maji nchini. Katika kikao hicho, Serikali ya Tanzania kupitia Wizara ya Maji na UNICEF zimekubaliana kuimarisha ushirikiano katika maeneo ya maji, usafi wa mazingira na afya (WASH) kwa lengo la kuboresha huduma za maji safi na salama pamoja na ustawi wa wananchi. Pande hizo pia zilijadili mikakati mbali...

MAKATIBU WAKUU WAKUTANA ARUSHA KUZUIA BIDHAA FEKI KUTOKA NJE YA KANDA

Image
Makatibu Wakuu wa Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) wanaosimamia masuala ya mtangamano wamekutana katika Makao Makuu ya Jumuiya hiyo jijini Arusha kwa ajili ya kukamilisha maandalizi ya Mkutano wa 48 wa Baraza la Kisekta la Mawaziri wa Biashara, Viwanda, Fedha na Uwekezaji (SCTIFI) ngazi ya mawaziri, unaotarajiwa kufanyika tarehe 4 Juni 2026. Kikao hicho cha Makatibu Wakuu, kinachofanyika kwa siku mbili kuanzia tarehe 2 hadi 3 Juni 2026, ni sehemu ya maandalizi ya mwisho ya mkutano wa mawaziri unaotarajiwa kutoa mwelekeo wa kisera na maamuzi yatakayochochea ukuaji wa biashara, maendeleo ya viwanda na ongezeko la uwekezaji katika Jumuiya, sambamba na kuimarisha ushindani wa uchumi wa kanda.   Makatibu Wakuu hao wamepokea na kujadili taarifa mbalimbali zilizowasilishwa na wataalamu kuhusu utekelezaji wa maamuzi ya mkutano uliopita wa SCTIFI. Miongoni mwa taarifa zilizojadiliwa ni pamoja na; taarifa Kamati ya Forodha, Kamati ya Viwango ya Afrika Mashariki, Kamati ya ...

WAZIRI MASAUNI AWATAKA VIJANA KUCHANGAMKIA TEKNOLOJIA NA FURSA ZA KIUCHUMI

Image
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Masauni amesema vijana wanapaswa kutumia fursa zinazotolewa na Serikali kwa kukuza ubunifu, kuongeza bidii katika kazi, kutumia teknolojia na kushiriki kikamilifu katika shughuli za kiuchumi hususan zilizo rafiki kwa Mazingira.  Mhe. Masauni amesema hayo katika Kongamano la Vijana lililofanyika jijini Dar es Salaam, Juni 2, 2026 ambalo ni sehemu ya Maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani ambapo kilele chake kitaifa yanafanyika Juni 5, 2026 mkoani Dodoma. Amesema, kongamano hilo ni jukwaa muhimu linalowaunganisha vijana na maadhimisho ya Siku ya Mazingira Duniani kwa kuwapa nafasi ya kushiriki katika mijadala, kujifunza kutoka kwa wataalam, kubadilishana uzoefu na kuibua suluhisho bunifu zinazoweza kutekelezwa kwa vitendo katika jamii zao. “Ninyi ndio nguvu kazi ya Taifa na nguzo muhimu katika mapambano dhidi ya uharibifu wa mazingira. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, vij...

​BILIONI 100 KILA MWEZI KULIPA MADENI, WAZIRI BALOZI OMAR AWALAINISHA WATUMISHI, WAKANDARASI NA WAZABUNI

Image
Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akiwasilisha bungeni jijini Dodoma, Mapitio ya Utekelezaji wa Mpango na Bajeti kwa mwaka wa fedha 2025/2026 na Mapendekezo ya Mpango na Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka 2026/2027, ambapo ameliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi trilioni 21.3 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27. Dodoma 2 Juni, 2026: Serikali kupitia Wizara ya Fedha imeliomba Bunge kuidhinisha jumla ya shilingi trilioni 21.3 kwa ajili ya utekelezaji wa majukumu ya Wizara hiyo pamoja na taasisi zake kwa Mwaka wa Fedha 2026/27. Akiwasilisha Mapendekezo ya Mpango na Bajeti bungeni, Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), alisema fedha hizo zitatumika kugharamia matumizi ya kawaida na maendeleo katika mafungu manane ya Wizara, ambapo kati ya fedha hizo, shilingi trilioni 19.4 zitatumika kwa matumizi ya kawaida huku shilingi trilioni 1.8 zikielekezwa kwenye miradi ya maendeleo. Alisema kuwa ka...

WAZIRI CHONGOLO NA BALOZI WA AUSTRALIA WAWEKA MKAKATI WA UTAFITI WA KILIMO

Image
​ DODOMA – Serikali za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Australia zimesisitiza kuendeleza ushirikiano wao wa kimkakati wa muda mrefu, unaolenga kuimarisha ushirikiano katika utafiti wa kilimo na ujenzi wa uwezo wa kiteknolojia nchini. ​Mazungumzo hayo yenye maslahi mapana yamefanyika leo tarehe 2 Juni, 2026, katika ofisi ndogo ya Wizara ya Kilimo mkoani Dodoma, kati ya Waziri wa Kilimo, Mhe. Daniel Chongolo (Mb) na Balozi wa Australia nchini Tanzania, Mhe. Jenny Da Rin. ​“Australia inashirikiana na Tanzania katika dhamira ya kuboresha maisha ya wakulima wadogo kupitia utafiti na usaidizi wa kiteknolojia. Tumefanya kazi kwa karibu na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) ili kuimarisha ujenzi wa uwezo, kuhakikisha kuwa usambazaji wa maji, usimamizi wa udongo, na matumizi ya miche inaimarishwa kiteknolojia ili kuongeza tija ya mazao na kuboresha maisha ya wakulima,” alisema Balozi Jenny Da Rin. ​Akikubaliana na kushukuru msaada endelevu wa Australia katika sekta ya kilimo, ...

RAIS SAMIA AMTEUA UMMY MWALIMU KUWA MSHAURI WAKE MPYA

Image
  DAR ES SALAAM – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amefanya uteuzi wa Mshauri wa Rais kuanzia leo, tarehe 02 Juni, 2026. ​Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Dkt. Moses Mpogole Kusiluka, aliyeteuliwa ni Bi. Ummy Ally Mwalimu ambaye anakuwa Mshauri wa Rais – Masuala ya Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto. Taarifa hiyo imesainiwa na Shaaban Kissu kwa niaba ya Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Ikulu.

SERIKALI KUIMARISHA MIFUMO YA USIMAMIZI WA MAAFA

Image
SERIKALI imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa ili kuhakikisha misaada ya kibinadamu inayotolewa inawafikia walengwa kwa wakati, ufanisi na kwa kuzingatia viwango vya kimataifa. Hayo yameelezwa leo tarehe 02 Juni, 2026 na Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na Wenye Ulemavu), Kanali Selestine Masalamado, wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura, mkoani Morogoro. Amesema utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wa dharura ni nguzo muhimu zinazowezesha kuokoa maisha ya wananchi walioathiriwa na maafa, kupunguza mateso ya waathirika na kuharakisha urejeshaji wa hali za kawaida katika maeneo yaliyoathirika. “Kwa kutambua umuhimu huo, Serikali imeendelea kuimarisha mifumo ya uratibu, kujiandaa na kukabiliana na maafa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha misaada inawafikia walengwa k...

DK. RICHARD MUYUNGI AKUTANA NA BALOZI WA NORWAY, MKAKATI MPYA WA MAPINDUZI YA MAZINGIRA YAANDALIWA

Image
  Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Dkt. Richard Muyungi amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Norway nchini Tanzania Mhe. Bi. Tone Tinnes. Mazungumzo hayo yamefanyika jijini Dar es Salaam Juni mosi, 2026. Katika mazungumzo hayo, Dkt. Muyungi ameishukuru Serikali ya Norway kwa ushirikiano wa muda mrefu waliouonesha kwa Serikali ya Tanzania katika sekta mbalimbali na kwa nyakati zote. Alisema kuwa Serikali chini Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua mchango wa nchi hiyo katika usimamizi mwa mazingira na kuhimili mabadiliko ya tabianchi. Dkt. Muyungi alitaja moja ya alama ya mchango wa Norway ni kuanzishwa kwa Kituo cha Study za Mabadiliko ya Tabianchi katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na kunzishwa kwa Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) chini ya Ofisi ya Makamu wa Rais. Kwa upande wake Balozi Mhe. Tonnes alisema kuwa Norway itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Makamu wa Rais katika masua mbalimbali yahusuyo sekta ya hifadhi ...

RIDHIWANI KIKWETE, ONDOENI URASIMU, ZINGATIENI KANUNI NA UTU KATIKA UTUMISHI WA UMMA

Image
  WAZIRI  wa Nchi, Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Ridhiwani Kikwete, amewataka Maafisa Tawala na Rasilimali Watu nchini kuzingatia kanuni, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma ili kuimarisha ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi. Waziri Kikwete alitoa wito huo jana wakati akifungua Mkutano wa Mwaka wa Maafisa Tawala na Rasilimali Watu uliofanyika katika Ukumbi wa Jenerali Mabeyo jijini Dodoma. Mkutano huo umewakutanisha Maafisa Tawala na Rasilimali Watu kutoka wizara, idara, taasisi za serikali zinazojitegemea pamoja na mamlaka za serikali za mitaa kwa lengo la kujadili changamoto mbalimbali za taaluma yao na kuweka mikakati ya namna bora ya kukabiliana nazo. Akizungumza katika mkutano huo, Waziri Kikwete alisisitiza umuhimu wa kuimarisha mawasiliano kati ya ofisi za washiriki na Ofisi ya Rais,  Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kurahisisha utatuzi wa changamoto zinazojitokeza katika maeneo yao ya kazi. A...