▪️Katavi KuKufuatia ukaguzi fanywa kwa wamiliki wa leseni wanaofanya uchimbaji kwenye mto na kuathiri mazingira, Waziri wa Madini *Mheshimiwa Anthony Mavunde (Mb)* atoa maelekezo ya kusimamishwa kwa shughuli za uchimbaji madini kwenye mto huo Mkoani Katavi. Ametoa kauli hiyo tarehe 13 Mei, 2026 alipofanya ziara ya ukaguzi wa shughuli za uchimbaji madini katika Manispaa ya Mpanda na Halmashauri ya Nsimbo Mkoani Katavi. "Mhe. Rais ametupa maelekezo mahsusi Wizara ya Madini kuhakikisha shughuli zote za uchimbaji zinafanyika kwa mujibu wa Sheria na zisilete athari kwenye mazingira. Tumeshuhudia sote kinachofanyika hapa ni kinyume na matakwa ya Sheria yetu ya Madini Sura 123" "Hivyo, naelekeza kuanzia leo shughuli zote za uchimbaji zisimame mpaka pale mtakapotekeleza wajibu wenu kama mlivyoelekezwa na Afisa Madini Mkazi wa Katavi kupitia barua aliyowaandikia. Pia, wamiliki wa leseni wasilisheni mpango wa kuhifadhi mazingira kabla ya kuanza shughuli za uchimbaji tena", al...