Posts

TANZANIA INAPOTEZA MITI 370,000 KILA MWAKA:NAIBU WAZIRI KWAGILWA NA NMB WAJA NA MKAKATI MPYA WA DIRA 2050

Image
Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Reuben Kwagilwa amewaomba wadau wa maendeleo kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali za kupanda miti ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Amesema hayo alipokutana na kufanya mazungumzo na watendaji wa Benki ya NMB kwa lengo la kuimarisha ushirikiano na kuweka mikakati ya pamoja ya hifadhi ya mazingira endelevu, kikao kimefanyika jijini Dodoma. Mhe. Kwagilwa alisema kuwa katika kufikia lengo la upandaji wa miti takriban bilioni mbili lililowekwa kupitia Dira 2050 zinahitajika nguvu za pamoja kati ya Serikali na wadau na kuendelea kuhamasisha jamii kupanda miti kwenye maeneo yao. Alisema ni lazima kuunganisha nguvu za pamoja kushirikiana ili kuifanya nchi kuwa ya kijani kwani hata katika kaulimbiu iliyotumika kwenye Siku ya Mazingira Duniani mwaka huu inasema ‘Dira 2050; Tuwajibike kukijanisha Tanzania’ ambayo inasisitiza umuhimu wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. “Karibu nusu ya eneo la nchi yet...

INDICATIVE EXCHANGE RATES TODAY JUNE 17th, 2026

Image
 

INDICATIVE EXCHANGE RATES TODAY JUNE 4th, 2026

Image
 

WFP KUENDELEA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KATIKA MASUALA YA USIMAMIZI WA MAAFA NCHINI

Image
Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula la Duniani (World Food Programme -WFP) limesema litaendeleza mashirikiano na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuhakikisha masuala ya menejimenti ya maafa yanaendelea kutekelezwa kwa tija na malengo yaliyokusudiwa kwa kuimarisha uwezo wa kitaalamu na Kiteknolojia kwa kutumia teknolojia za kisasa. Hayo yameelezwa na Naibu Mkurugenzi wa WFP Tanzania Bi. Christine Mendes wakati wa ufunguzi wa warsha ya zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wakati wa dharura inayoendelea mkoani Morogoro. Bi.Christine alisema ushirikiano hususan katika kuwezesha utekelezaji wa Mradi wa Field-Based Preparedness Project (FBPP), ambapo katika kipindi cha miaka miwili iliyopita, mradi huo umechangia kwa kiasi kikubwa kuimarisha uwezo wa taifa katika sekta ya utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji. Aidha, alieleza kuwa zoezi la uigaji la uratibu wa utoaji wa misaada ya kibinadamu na usafirishaji wak...

SERIKALI YAENDELEA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA BARABARA ZA WILAYA KUIMARISHA UCHUMI: MSIGWA

Image
  Mwanza Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya barabara nchini kwa kupunguza barabara za changarawe na kujenga barabara za lami katika wilaya mbalimbali, hatua inayolenga kuwawezesha wananchi kuinuka kiuchumi kupitia shughuli za usafirishaji. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa, alipokuwa akizungumza na Maofisa Uhusiano na Mawasiliano Serikalini wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Chama cha Maofisa Mawasiliano Serikalini (TAGCO) unaoendelea jijini Mwanza. Msigwa amesema maofisa Mawasiliano wanapaswa kuhakikisha wananchi wanapata taarifa sahihi kuhusu miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali kwa kuwa miradi hiyo ni ya manufaa kwa wananchi wenyewe. “Sisi ndiyo tunaobeba taswira ya Serikali. Tunapaswa kuwaonesha wananchi fursa zilizopo kutokana na uwekezaji mkubwa wa miundombinu unaofanywa na Serikali,” amesema. Ameongeza kuwa Serikali imejenga barabara za mzunguko zenye urefu wa kilomita 56 k...

RAIS SAMIA AKUTANA NA VLADIMIR PUTIN MOSCOW, WAWEKA MKAKATI MZITO WA DIPLOMASIA

Image
MOSCOW, URUSI – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo tarehe 03 Juni, 2026, amewasili katika Ikulu ya Kremlin jijini Moscow nchini Urusi kwa ajili ya ziara ya kiserikali yenye lengo la kuimarisha uhusiano wa kidiplomasia na kiuchumi kati ya nchi hizo mbili. ​Mara baada ya kuwasili Ikulu hapo, Rais Samia alilakiwa na mwenyeji wake, Rais wa Shirikisho la Urusi, Mhe. Vladimir Putin, ambapo viongozi hao wawili walisalimiana na kupiga picha ya pamoja kabla ya kuelekea kwenye meza ya mazungumzo. ​Katika ziara hiyo, Rais Samia ameongoza ujumbe mzito wa viongozi na wataalamu kutoka Tanzania katika mazungumzo rasmi na Rais Vladimir Putin pamoja na ujumbe wake wa Serikali ya Urusi. ​Mazungumzo hayo yaliyofanyika ndani ya Ikulu ya Kremlin yamelenga kuimarisha ushirikiano wa muda mrefu katika nyanja za kimkakati ikiwemo biashara, uwekezaji, teknolojia, na diplomasia ya kimataifa, huku yakifungua milango mipya ya maendeleo kwa pande zote mbili.

MAAFISA 2,028 KUPANDISHWA VYEO: IDARA YA UHAMIAJI YAWEKA REKODI MPYA SERIKALINI

Image
  ‎Katika jitihada za kuendelea kuimarisha utendaji kazi wa taasisi za umma na kuongeza tija katika utoaji wa huduma kwa wananchi, Serikali imeendelea kutekeleza sera ya kuwathamini na kuwatambua watumishi kupitia upandishaji vyeo kulingana na sifa, uzoefu na utendaji wao wa kazi. Hatua hiyo imeendelea kuleta matokeo chanya katika Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi na taasisi zake, ikiwemo Idara ya Uhamiaji. ‎Kwa mujibu wa Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, jumla ya watumishi 9,689 wa Wizara na taasisi zake walipandishwa vyeo.  ‎Kati ya hao, watumishi 693 wa Idara ya Uhamiaji walinufaika na hatua hiyo, jambo linalodhihirisha dhamira ya Serikali ya kuendelea kuwatambua watumishi wanaotekeleza majukumu yao kwa uadilifu, weledi na kujituma. ‎Katika mwaka wa fedha 2026/27, Serikali imepanga kuendelea kuimarisha ustawi wa watumishi wake kwa kuwapandisha vyeo jumla ya watumishi 23,089 wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nch...