MABADILIKO YA RATIBA YA TRENI YA ABIRIA YA MUKUBA YA MIPAKANI.

Taarifa hii inawatangazia wasafiri wetu pamoja na umma kwa ujumla kuwa Treni ya Mukuba ya Mipakani, ambayo ilikuwa imepangwa kuondoka Dar es Salaam kuelekea New Kapiri Mposhi siku ya Ijumaa tarehe 15 Mei 2026 saa 09:50, alasiri, sasa itaondoka siku ya Jumamosi tarehe 16 Mei 2026 saa 09:50, alasiri.

Mabadiliko haya ya ratiba yamesababishwa na kuchelewa kwa treni kuwasili Dar es Salaam kutoka New Kapiri Mposhi kutokana na changamoto mbalimbali za kiufundi na kiuendeshaji zilizojitokeza katika kipindi cha wiki hii.

Tunawashukuru kwa dhati wateja wetu kwa uvumilivu, uelewa na ushirikiano wao wanapoendelea kutuunga mkono katika kipindi hiki cha maboresho na uhuishaji wa reli.

Tunaendelea kuwa na imani kuwa reli yenu itaibuka ikiwa imara zaidi na yenye uwezo mkubwa kama mfumo wa usafiri ulio salama, wa kuaminika na wenye gharama nafuu ambao mnaweza kuutegemea wakati wote.

Kwa taarifa za haraka kuhusu ratiba za treni na huduma za tiketi, tafadhali wasiliana kupitia namba zilizo kwenye picha husika.

Comments

Popular posts from this blog

RESIDENTS OF IYAGABUYAGA-BUSEGA URGED TO RESPECT WILDLIFE CONSERVATION LAWS

MATIVILA URGES CONTRACTOR TO DELIVER MOHORO BRIDGE ON SCHEDULE